Inavyoonekana, kadiri mtu anavyozidi kupata elimu ndivyo anavyozidi kudharau uwepo wa Shetani na uwepo wa Mungu pia. Lakini, kwa upande mwingine, ndivyo anavyoonekana hajasoma sana na ndivyo Shetani anavyozidi kulaumiwa kwa kila dhambi inayotendeka. Kuna elimu ya kidunia na kuna elimu ya kidini. Huwezi kutawala dunia bila elimu ya kidunia, kwa sababu Shetani anajua ukiipata elimu hiyo hutajua kama yupo; na huwezi kutawala dunia bila elimu ya kidini, kwa sababu Mungu anajua ukiipata elimu hiyo utajua kama yupo. Hivyo, utamdharau Mungu ukipata elimu ya kidunia, utamheshimu Mungu ukipata elimu ya kidini.